Kufunguliwa Kwa Dirisha la Usajili 2023/24

TAVA imetangaza ufunguzi wa dirisha la usajili kwa msimu wa mashindano wa 2023/24, likianza tarehe 13/11/2023 hadi 12/12/2023. Mfumo wa usajili umepitia maboresho ya kanuni ili kukidhi mahitaji na unahusisha vilabu, makocha, wachezaji, waamuzi, na taasisi nyingine.

3 min

Chama Cha Mpira wa Wavu Tanzania – TAVA kinawataarifu wadau wote kuwa Dirisha la usajili kwa msimu wa mashindano kwa mwaka 2023/24 unafunguliwa tarehe 13/11/2023 saa moja asubuhi. Mfumo huu wa usajili utakuwa wazi kwa siku thelathini (30) hadi tarehe 12/12/2023 saa sita usiku. Sambamba na kufunguliwa dirisha la usajili, kumefanyika maboresho ya Kanuni za Usajili za Mwaka 2022 Toleo la Mwezi Februari ili kukidhi mahitaji ya wakati. Viongozi na wadau wote wanaelekezwa kuzisoma nakuzielewa kanuni hizo kabla ya kufanya usajili. Mfumo wa usajili utakuwa na mambo yafuatayo;

  1. Mfumo huu wa usajili utafanyika kwenye tovuti ya TAVA kupitia linki (anuani) maalumu
  2. Taarifa zote za usajili wa msimu uliomalizika 2022/23 zimefutwa.
  3. Mfumo wa usajili utahusisha Klabu, Kocha, Wachezaji, Waamuzi, Taasisi binafsi (Foundation/Academy), na Shule za kukuza vipaji/ Vitalu au Vituo.
  4. Mfumo wa usajili utakuwa na mipaka ya matumizi kulingana na wahusika;

Kamati kuu ya TAVA inawaomba wenyeviti wa mikoa kuhakikisha taarifa hizi zinawafikia viongozi wote wa Vilabu, Makocha na Waamuzi na kuratibu ama kufuatilia utekelezaji wake ikiwa ni pamoja nakuwasainia viongozi wa vilabu na taasisi barua za utambulisho ili kukamilisha zoezi hili kwa wakati. Hakutakuwa na Klabu, Taasisi, Kitalu wala muhusika yoyote atakayesajiliwa pasipokuwapo na ufahamuwa uongozi wa Mkoa. Kwa changamoto zozote za kimfumo wasiliana na namba zifuatazo: 0764837005 au 0762550211.

Bonyeza anuani ya usajili ya TAVA kuingia kwenye mfumo - https://register.tvf.or.tz/

More News

Blog details image
Usajili
Arrow Icon

Kufunguliwa Kwa Dirisha La Usajili Kwa Vituo Na Shule Za Kulelea Watoto, Taasisi Binafsi, Makocha Na Waamuzi

Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania – TVF, linawataarifu wadau wote kuwa dirisha la usajili kwa Vituo na Shule za kulelea Watoto, Taasisi binafsi, Makocha na Waamuzi limefunguliwa kuanzia leo tarehe 2/2/2024 hadi tarehe 16/2/2024.

Blog details image
National Team
Arrow Icon

Wachezaji Waliochoguliwa Kuwakilisha Timu ya Taifa Katika Mashindano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki 2024

Orodha ya Wachezaji Waliochoguliwa Kuwakilisha Timu ya Taifa Katika Mashindano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki 2024

Blog details image
Usajili
Arrow Icon

Kanuni za Ligi na Usajili 2023/24

TAVA yaendelea kuboresha sheria na kanuni zinazoongoza mpira wa wavu nchini - ikigusia msimu wa mashindano, mfumo, mahitaji na ada za usajili kwa mwaka 2023.